{"id":1216612,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1216612/?format=json","text_counter":369,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Wale ambao waliiandika Katiba hii, na ni sisi Wakenya, hatukumaanisha miungano ya aina hii. Ndiposa Halmashauri ya Usajili wa Mashirika ambayo yalikuwa yamekataa kusajili miungano kama hii yakasimama kidete na yakakataa. Hata hivyo, mambo haya yalipelekwa katika Korti yetu la Upeo na yakaidhinishwa."}