{"id":1221365,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1221365/?format=json","text_counter":59,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"The Senate Minority Leader","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":" Bw. Spika, mimi sipingi uamuzi wako. Lakini, taratibu za Bunge la Seneti zinasema kuwa ikiwa kuna Wabunge ambao wamesema, “tafadhali Bw. Spika, niko na Hoja ya nidhamu, kwa kawaida, huwa unawapatia nafasi hawa Maseneta waweze kuweka wazi Hoja zao za nidhamu, ili ukifanya uamuzi wako, unaufanya kwa pamoja, halafu tuendelee. Hata Sen. (Dr.) Khalwale alitaka kuzungumza. Hiyo ndiyo taratibu ya Bunge la Seneti."}