{"id":1225581,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1225581/?format=json","text_counter":667,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"The Senate Minority Leader","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Kitendo hicho cha kupiga risasi ni kinyume cha sheria. Askari hawaruhusiwi kupiga watu risasi. Askari hawaruhusiwi kurusha hata hiyo teargas ambayo inarushwa wakati kuna fujo. Lakini haya yalikuwa maandamano ambayo yalikuwa yanafanywa katika nchi nzima kulingana na ile barua pepe tuliyopeleka kwa mkuu hapa Nairobi ili watu waweze kufanya maandamano ya amani."}