{"id":1225591,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1225591/?format=json","text_counter":677,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Cha muhimu ni kwamba, Kiongozi wa Walio Wachache ndani ya Bunge la Kitaifa na Kiongozi wa Walio Wachache ndani ya Bunge la Seneti, Mbunge wa Kilifi South, Ken Chonga, pamoja na Mbunge wangu wa Malindi, mama wa Kiisalmu, wakati huu ambapo watu wanazingatia Al Hayat, kuenda kuomba Mungu na kuweza kuheshimu dini ya Kiislamu, alikuwa amevaa buibui na hijab alishikwa bila heshima; akavuliwa hijab na buibui."}