{"id":1227253,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1227253/?format=json","text_counter":405,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wafula","speaker_title":"","speaker":{"id":348,"legal_name":"Davis Wafula Nakitare","slug":"davis-nakitare"},"content":"Bi. Spika wa Muda, nadhani nchi nzima inasikiliza mjadala huu na pande zote zina haki kutoa hoja ambazo Wakenya wanaskiliza kwa makini. Ninaelewa fika yale mambo ambayo yanashinikiza ndugu zetu walio kwenye upande wa wachache kwenye Bunge. Ni sawa kwa sababu sheria inawapa uwezo wa kusema yale wanasema. La muhimu ni kuwa kule tunakotoka, watu wanataka kuona Mawaziri wakiwajibika."}