{"id":1227254,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1227254/?format=json","text_counter":406,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wafula","speaker_title":"","speaker":{"id":348,"legal_name":"Davis Wafula Nakitare","slug":"davis-nakitare"},"content":"Sen. Sifuna umetaja vipengele ambavyo kwako ama kwa wale walio kwenye upande wa wachache, sheria hizi zinawangandamiza ama kuwafinya Maseneta wasijieleze fika mbele ya umma. Ni sawa na tuna nafasi ya kubadilisha. Kile tunasema kama walio upande wa Serikali ni kwamba Mawaziri ambao wamechaguliwa na Mhe. Rais wanapofanya kazi yao hapa Kenya ni lazima wawajibike. Ni vyema wajieleze na kudhihirisha kwamba Kenya ni yetu sisi sote."}