{"id":1227255,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1227255/?format=json","text_counter":407,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wafula","speaker_title":"","speaker":{"id":348,"legal_name":"Davis Wafula Nakitare","slug":"davis-nakitare"},"content":"Bi. Spika wa Muda, kwa mfano, juzi tumeona Baraza la Mawaziri. Kwenye vyombo vya habari, kulikuwa na taarifa kwamba kutakuwa na ubinafsishaji wa mashirika ya Serikali zikiwemo hoteli. Hiyo ni sawa lakini kuna Mawaziri ambao tanangoja hapa. Waziri husika anafaa kuja na kutueleza aliuliza nani ruhusa ya kubinafsisha mali ya Serikali kwa sababu sisi ni viongozi ambao tunawaakilisha Wakenya."}