{"id":1229169,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1229169/?format=json","text_counter":274,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bunge la Seneti likapeleka Kamati kwenda kuchunguza na ikapatikana kwamba ni kweli waliwakusanya wale randa randa wa mjini wote na wakaenda wakawatupa msituni. Ni mambo ambayo yamefanyika. Ni lazima tuwakemee sisi kama Maseneta katika nchi yetu ya Kenya."}