{"id":1231840,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1231840/?format=json","text_counter":229,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Asante, Bw. Spika, kwa kunipa fursa hii. Nilileta Kauli hapa kuhusu kusitishwa kwa huduma za umeme katika Coast General Teaching and Referral Hospital katika Kaunti ya Mombasa. Hadi leo, sijapata ripoti yoyote wala Mwenyekiti wa Kamati ya Afya hakuitaji Kauli hiyo katika ripoti yake ya miezi sita tangu Kamati ilipoanza kazi mwezi wa Oktoba mwaka jana."}