{"id":1234452,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1234452/?format=json","text_counter":222,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wambua","speaker_title":"","speaker":{"id":13199,"legal_name":"Enoch Kiio Wambua","slug":"enoch-kiio-wambua"},"content":"Asante, Bw. Naibu Spika. Nimemskiza Seneta mwenzangu, Seneta wa Laikipia, Sen. Kinyua. Kwa mara kadhaa amerudia maneno “ndege kutembelea Mombasa”, “kuzuru na kutembelea” pia. Jinsi ninavyoelewa Kiswahili, watu hutembelea sehemu fulani, lakini ndege hutua. Sijui kama Seneta wa Laikipia anaongea kuhusu ile ndege sisi tunafahamu ama ni ndege zingine."}