{"id":1234715,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1234715/?format=json","text_counter":485,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Madzayo","speaker_title":"The Senate Minority Leader","speaker":{"id":679,"legal_name":"Stewart Mwachiru Shadrack Madzayo","slug":"stewart-mwachiru-shadrack-madzayo"},"content":"Bw. Spika wa Muda, mimi kama Seneta wa Kaunti ya Kilifi, ninasikitika. Niko pamoja na watu wote ambao wamepoteza wapendwa wao. Tunawaombea Mwenyezi Mungu. Lakini, jambo kama hili ni lazima lichunguzwe, lifikishwe mwisho na wale watakaopatikana walizembea kwa kazi zao, Rais achukue hatua ya kuwafuta kazi."}