{"id":1240150,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1240150/?format=json","text_counter":373,"type":"speech","speaker_name":"Kaunti ya Nakuru, UDA","speaker_title":"Mhe. Liza Chelule","speaker":null,"content":" Asante sana, Mhe. Spika, kwa kunipatia nafasi nielekeze swali langu kwa Waziri wa Elimu. Kwa wale wanafunzi ambao wamefanya mitihani ya shule ya upili, sijui kama ana habari kwamba kila wakati watoto hawa wakienda kuchukua stakabadhi zao shuleni wanakatazwa kama hawajamaliza kulipa karo ya shule. Asante, Mhe. Spika."}