{"id":1244903,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1244903/?format=json","text_counter":177,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Kwa hivyo, kuna haja ya kubadilisha ama kurekebisha sheria ya fedha, yaani, Public Finance Management (PFM) Act kuhakikisha kwamba bunge la kaunti lina fedha zake mbali na zile fedha ambazo ziko katika serikali ya kaunti. Hii ni kwa sababu serikali ya kaunti mara nyingi wakiitisha pesa, wanapunguziwa ama wanatolewa pesa kidogo kidogo ili kuhakikisha kwamba kazi zao zinahujumiwa."}