{"id":1254898,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1254898/?format=json","text_counter":125,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Kuna zile pombe za kitamaduni zinazokubalika zisizoathiri afya ya watu. Lakini, hata hivyo, serikali imejizatiti na kujitolea kupigana na pombe haramu. Naunga mkono Taarifa hii kwa sababu ukitembea sehemu za Laikipia, utapata vijana wamelala na hawafanyi chochote. Naunga mkono serikali kuendelea kupigana na hizi pombe haramu lakini wasiwavamie wananchi wasiokuwa na makosa yeyote."}