{"id":1262881,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1262881/?format=json","text_counter":30,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Asante, Bw. Spika. Nataka kuungana nawe kuwakaribisha ndugu zetu waheshimiwa kutoka Kaunti ya Nyandarua. Kaunti ya Nyandarua ni jirani na Kaunti ya Laikipia. Seneta wao ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ardhi, Mazingira na Mali Asili. Ni kiongozi ambaye tunatambua kwenye shughuli za kikazi. Ni mtu anayefanya kazi nzuri kama Seneta."}