{"id":1267877,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1267877/?format=json","text_counter":92,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wafula","speaker_title":"","speaker":{"id":348,"legal_name":"Davis Wafula Nakitare","slug":"davis-nakitare"},"content":"Asante, Bw. Spika, kwa nafasi hii. Jambo tunayozungumzia sasa inaweka Mawaziri katikati ya jiwe na pahali pagumu. Yule ambaye aliwateua na anawaamini kwa uchapakazi na uadhilifu wao ameona kwa hekima yake kuwapa nafasi kusafiri naye katika nchi za ng’ambo kutetea nafasi na hadhi ya nchi ya Kenya na mustakabadhi wa Wizara zao na nchi wanayokwenda."}