{"id":1278196,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1278196/?format=json","text_counter":216,"type":"speech","speaker_name":"Likoni, ODM","speaker_title":"Hon. Mishi Mboko","speaker":null,"content":"Vile vile, kwa sasa tunaona miradi mikubwa mikubwa ya Serikali inayodhihirika katika sehemu tofauti tofauti. Kwa mfano, kule kwangu kuna mradi wa Dongo Kundu Bypass. Ni barabara. Pia, kuna ile Special Economic Zone. Wakaazi wanaoishi pale wamekuwa hapo kwa miaka mingi. Wameishi hapo kana kwamba ni ardhi ya Umma pasi na kuwa na hatimiliki. Sasa Serikali imetumia compulsory land acquisition. Kwamba, Serikali itachukua ile ardhi ili kutengeza ule mradi wa Umma utakaofanyika pale."}