{"id":1278895,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1278895/?format=json","text_counter":296,"type":"speech","speaker_name":"Keiyo South, UDA","speaker_title":"Hon. Gideon Kimaiyo","speaker":null,"content":"Jambo la pili ni kuhusu njia itakayotumika kumtambua mwanafunzi anayestahili kulipiwa karo na ufadhili. Wanasema watatumia tarakilishi. Yule mtu ambaye ako mashinani— kwa mfano, mahali ninakotoka kule Kerio Valley—atatoa wapi tarakilishi. Hiyo ni njia ya kumfungia asipate msaada wa ufadhili katika chuo kikuu."}