{"id":1279252,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1279252/?format=json","text_counter":309,"type":"speech","speaker_name":"Kwale County, ODM","speaker_title":"Hon. Fatuma Masito","speaker":null,"content":" Ahsante sana, Mhe. Spika. Nimesikia Waziri amesema kumetengwa pesa ya kukarabati uwanja wa ndege wa Ukunda, sehemu ambayo ina watalii wengi sana. Je, anafahamu kuwa wananchi wanaotoka sehemu ile bado hawajapata fidia kwa kunyang’anywa uwanja ule? Hao ni wananchi wa sehemu ya Mkwakwani, Ukunda."}