{"id":1283163,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1283163/?format=json","text_counter":180,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Bw. Naibu Spika, tumeketi na Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu. Ni desturi yetu wanafunzi wanapokuja hapa, ili kuwapa motisha, tunawataja kwa majina. Najua shughuli ya leo ni ya dharura, lakini ni vizuri kuwataja kwa majina ndiposa tuwape motisha. Bw. Naibu Spika, naskia watu wengi wakisema mambo ni magumu. Lakini, tuwape motisha viongozi wa kesho."}