{"id":1286172,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1286172/?format=json","text_counter":377,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Mungatana, MGH","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Kwa hivyo, ingekuwa muhimu wananchi wapewe sauti kwa jinsi ambavyo pesa zao zinatumika. Wananchi wasikose katika hizo kamati za hospitali, sub-countymanagement committees na ile ya kaunti. Tukifanya hivyo, wananchi wote watajua kiasi cha pesa kilichokusanywa mwezi fulani na hata kiasi ambacho kimetumika kununua madawa, sindano na bandages. Wananchi watatosheka na usimamizi wa hizi kaunti. Kwa hayo machache, ninaomba kuunga mkono."}