{"id":129683,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/129683/?format=json","text_counter":71,"type":"speech","speaker_name":"Ms. Leshomo","speaker_title":"","speaker":{"id":379,"legal_name":"Maison Leshoomo","slug":"maison-leshoomo"},"content":"Bw. Spika, Waziri Msaidizi amesema ya kwamba hana habari kuhusu huo ugonjwa. Hata hivyo, kuna dhibitisho tosha kuwa watu watatu walifariki kutokana na ugonjwa wa meningitis. Watu hawa wanajulikana kuwa walikufa kutokana na ugonjwa huu. Watu wengi wanakufa kutokana na ugonjwa huu. Waziri Msaidizi atafanya nini kudhibitisha ukweli wa mambo haya?"}