{"id":1323854,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1323854/?format=json","text_counter":182,"type":"speech","speaker_name":"Kitui Kusini, JP","speaker_title":"Mhe. (Dr) Rachael Nyamai","speaker":null,"content":"Sisi, kama Wakenya, tuna nchi na lugha nzuri ya kiswahili ambayo tunafaa kujivunia na kuipenda. Nimeangalia Ripoti hii kwa makini. Nimeona kwamba Wabunge ambao wako kwa Kamati hii pia wameangalia vile ambavyo nchi zingine zinaangalia utamaduni wao na kuweza kuchunga watu wao wasipoteze vitu vyao ambavyo ni vya kiasili."}