{"id":1341002,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1341002/?format=json","text_counter":272,"type":"speech","speaker_name":"Mombasa County, ODM","speaker_title":"Hon. Zamzam Mohammed","speaker":null,"content":" Ahsante sana Bi Spika wa Muda. Sote tunajua kuwa NHIF itagawanywa kuwa vitengo vitatu. Mumeweka mipango ipi kwa wafanyakazi wanaofanya kazi katika Idara ya NHIF? Tunasikia kuwa wengine watafutwa kazi. Hawa ni wafanyakazi wa Serikali na uchumi wetu si mzuri hivi sasa. Je, mmepanga vipi kuhusu wafanyakazi hawa? Ahsante sana."}