{"id":1349958,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1349958/?format=json","text_counter":302,"type":"speech","speaker_name":"Mombasa, ODM","speaker_title":"Hon. Zamzam Mohammed","speaker":null,"content":" Asante sana, Mhe. Spika. Ninataka pia kuongeza usemi wangu kwenye uamuzi ulioutoa leo. Ni haki kwa Wakenya kuona viongozi wao wakiwa wamevaa mavazi rasmi, ambayo ndiyo mavazi ya Bunge. Tusidanganyane hapa kuwa my dress, my choice. Kuna nguo zingine zinakuwa za mvuto. Zinasumbua watu kufocuss ndani ya Bunge."}