{"id":1395349,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1395349/?format=json","text_counter":205,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Olekina","speaker_title":"","speaker":{"id":407,"legal_name":"Ledama Olekina","slug":"ledama-olekina"},"content":"Ningependa kumshukuru Sen. Faki ambaye ametilia maanani yale mambo ninayozungumzia hapa kuhusu afya ya Wakenya. Je, itakuwa ni ungwana ikiwa ukienda kule Jaribuni Kilifi County, ukisimama na kuhesabu wanaume ni kama 20 peke yake, lakini mtoto ni mmoja. Vile amesema, hii vumbi inaharibu mbegu ya mwanaume. Hicho ni kitu kinanikera sana. Ndivyo ninasema, ningemshawishi mwenzangu Kiongozi wa Walio Wachache alete Hoja hapa katika Bunge hili ili tuweze kuchunguza. Jambo hili sio jambo la kuchezewa. Ukiona watoto wanaokuwa vipofu, wagonjwa, na wazazi wao hawana pesa ya kuwapeleka hospitali, tunakuwa kweli fair? How do you say ‘ fair ’ in Kiswahili? Asante."}