{"id":1411869,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1411869/?format=json","text_counter":261,"type":"speech","speaker_name":"Malindi, ODM","speaker_title":"Hon. Amina Mnyazi","speaker":null,"content":"Mimi naunga mkono ili hii tume iweze kuongezewa muda wa utendakazi. Leo hii ninavyozungumza niko na furaha na nataka kuwatangazia Wabunge wenzangu, kwamba sasa hivi nimetoka katika ofisi za hii tume kufuatilia maswala ya uwanja wa ndege kule Malindi. Mpaka dakika hii, kuna watu hawajaweza kulipwa ili ule uwanja upanuliwe."}