{"id":1421010,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1421010/?format=json","text_counter":200,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Sen. Olekina amesema kuwa ile vumbi ya madini inaleta athari mbalimbali kwa jamii. Moja ya hizi athari ni upungufu wa nguvu za kiume kwa watu wanaokaa sehemu zile. Hata ukiangalia, kuna hukumu iliyotolewa dhidi ya Clinker. Hukumu iliyotolewa kwa wakazi wa eneo la Uhuru Mombasa ni kwamba Clinker ilikuwa inaathiri uwezo wao wa kufanya tendo la ndoa na bibi zao. Kwa hivyo, madini yanayo chimbwa kule, baadhi ya athari zake ni hizo. Asante."}