{"id":1424504,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1424504/?format=json","text_counter":252,"type":"other","speaker_name":"","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Korti iliamua tuandae kamati ya upatanishi. Tunaendelea na jambo hili na pia tutashirikiana na viongozi wa Nandi ili haki ipatikane. Nahakikishia Bunge la Seneti kwamba tuna ufahamu wa jambo hili, na tunaendelea kufuatilia haki za wananchi kwenye sehemu ya Kerebe, Kaunti ya Nandi. Asante, Bi. Spika wa Muda ."}