{"id":1425342,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1425342/?format=json","text_counter":279,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Kwanza kabisa, Bw. Spika wa Muda, ningependa kuipongeza Kamati yako ya Haki, Masuala ya Kisheria na Haki za Kibinadamu kwa kupendekeza kwamba Seneti ikatae Mswada huu. Najua kwamba katika kamati yako, kuna Maseneta wenye tajriba kubwa. Kuna mawakili ambao wamesoma na kushauri Bunge hili kwamba Mswada huu hauna nia njema kwa Seneti."}