{"id":1425353,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1425353/?format=json","text_counter":290,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bw. Spika wa Muda, tunapinga Mswada huu kwa sababu ni lazima Mabunge yote mawili yatoe wawakilishi, wakae chini na waangalie ni mambo gani yatawekwa kwa Mswada huu ili ukubalike katika Bunge zote mbili. Hatuwezi kutunga sheria ya kusimamia Bunge la Seneti wakati Maseneta hawajahusishwa na utungaji wa sheria hiyo."}