{"id":1425698,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1425698/?format=json","text_counter":52,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Maanzo","speaker_title":"","speaker":{"id":13589,"legal_name":"Maanzo Daniel Kitonga","slug":"maanzo-daniel-kitonga"},"content":"Niko na swali, Bw. Naibu Spika. Jambo kubwa sana ambalo lilikuwa limeleta shida ni magonjwa ya Kahawa, hasa kule Makueni sehemu za Mbitini, Mbooni, Kilungu na Machakos upande wa Kangundo ambako kahawa hukuzwa. Ni jambo gani utafanya uhakikishe ya kwamba yale magonjwa hayatarudi tena? Siku hizi kahawa ya Makueni haizai sana kwa sababu ya ile mbolea ambayo huwekwa."}