{"id":144254,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/144254/?format=json","text_counter":147,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Wamalwa","speaker_title":"","speaker":{"id":148,"legal_name":"Eugene Ludovic Wamalwa","slug":"eugene-wamalwa"},"content":"Hoja ya nidhamu, Bw. Naibu Spika. Waziri Msaidizi tayari amekubali kwamba bomu hili lilitokana na mazoezi ya wanajeshi wa Kenya na pia, lilikuwa la wanajeshi wa Kenya. Je, Waziri Msaidizi anaweza kuliambia Bunge hili eti familia ya kijana aliyeathirika haitalipwa fidia?"}