{"id":144263,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/144263/?format=json","text_counter":156,"type":"speech","speaker_name":"Mr. Musila","speaker_title":"","speaker":{"id":94,"legal_name":"David Musila","slug":"david-musila"},"content":"Bw. Naibu Spika, utakubaliana nami kwamba hiyo si Hoja ya nidhamu bali ni swali. Nimesema kwamba Serikali inafanya mipango kutuma wanajeshi katika sehemu hizo zote kwa minajili ya kuzifagia na kutafuta njia za kuondoa vifaa hivyo vyote. Naomba wananchi washirikiane na wanajeshi wetu wakati huo ukifika ndiposa tuweze kumaliza shida hii kabisa."}