{"id":1442729,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1442729/?format=json","text_counter":137,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Naomba kusahihisha kwamba Mombasa hakuna simba. Huwezi kupata simba kwa Municipal Children ama mahali popote Mombasa. Kwa hiyo, msiwe na hofu kuja. Pili, nachukua fursa hii kwa niaba yangu binafsi na waakazi wa Mombasa, kupeleka rambirambi kwa jamaa, marafiki na ndugu wote ambao waliuliwa wakati wa maandamano ya jana, tarehe 25 na siku nyingine zilizokuwa na maandamano."}