{"id":1446012,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1446012/?format=json","text_counter":146,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Mungatana, MGH","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Bw. Naibu Spika, Ripoti hii inatukumbusha kwamba Bunge la Seneti kupitia kamati ya afya wanasisitiza kuwa pesa za wananchi pale Kenya Medical Supplies Authority (KEMSA) na katika vituo vyote vya Serikali zitumike vizuri. Hizi pesa sio zetu; ni za wananchi hawa na ni haki kuwaeleza kila siku. Kama wewe ni gavana na unaenda hospitali ili kusimamisha good services lakini umepata nusu, robo au hujapata pesa zozote, basi waelezee wananchi."}