{"id":1474284,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1474284/?format=json","text_counter":186,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Munyi Mundigi","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Nikimalizia, nataka kumjuza Seneta wa Nairobi kuwa tukiwa hapa kama Maseneta ni vyema tuwe na heshima kwa Serikali kwa sababu tuko kwa Serikali ya Muungano. Kama Seneta mzima hawezi kumheshimu Rais wa Kenya, nataka kumwambia Seneta wa Nairobi ya kwamba Rais sio Ruto. Anaitwa Rais William Samoei Ruto. Sio kumtaja jina tu. Ni sharti umheshimu kwa sababu hata wewe kesho unaweza kuwa rais."}