{"id":1476017,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1476017/?format=json","text_counter":406,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Mungatana, MGH","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Utumizi mbaya wa fedha uko na njia mwafaka wa kushughulikiwa. Kuna sheria inayopaswa kufuata. Wanaohusika watakamatwa. Uchunguzi utafanywa na watakaopatikina na hatia watachukuliwa hatua za kisheria. Hivyo basi, swala hili la utumizi mbaya wa fedha za kaunti isiwe sababu ya kupunguza fedha zinazoenda kwa upande wa ugatuzi."}