{"id":1476058,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1476058/?format=json","text_counter":447,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bw. Spika wa Muda, kwa hivyo, ipo haja ya kurekebisha Katiba ili ile asilimia inayotumika iwe ya mapato ya mwaka wa sasa. Hii ni kwa sababu serikali imenuia kukusanya hizi pesa katika kaunti. Kwa hivyo, hatuoni sababu ya takwimu za mwaka huu kutotumika kuhakikisha kwamba pesa zinapatikana."}