{"id":1476065,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1476065/?format=json","text_counter":454,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bw. Spika wa Muda, ningependa tu kugusia mambo mawili ambayo yameangaziwa leo katika vyombo vya habari. Pesa nyingi zinatumika kwa mambo mengi ambayo siyo ya msingi kimaendeleo katika kaunti zetu. Tumeambiwa, kwa mfano, Kaunti ya Kakamega, chai na mandazi na mambo mengine yasiyo muhimu, yametumia karibu shilingi milioni 522; Kaunti ya Nakuru imetumia shilingi milioni 400 na Bungoma vilevile. Ijapokuwa sikuiona ya Mombasa County labda sisi hatutumii mahamri sana."}