{"id":1477747,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1477747/?format=json","text_counter":92,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Kinyua","speaker_title":"","speaker":{"id":13202,"legal_name":"John Kinyua Nderitu","slug":"john-kinyua-nderitu-2"},"content":"Badala ya shamba lile kuleta afueni kwa ufanyi biashara wa Serikali kama kuweka ng’ombe wa nyama, unapata hilo shamba linakua donda sugu kwa wakaaji wa sehemu ile. Hii ni kwa sababu, wafugaji na wezi wanajificha kule, wakiwavizia na wakiwavamia wakaaji wa kule ambao hawana hatia yeyote."}