{"id":1491307,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1491307/?format=json","text_counter":78,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Hii ni kwa sababu FIFA kule Zurich watakuja mbio kutetea FKF hapa nchini. Ni muhimu kwamba wakati huu, tunapojipanga kwa kura za FKF, mambo yote ya sheria ifuatwe ili tuondoe wale walowezi ambao wamekamua huyu ng’ombe wa FKF kwa muda mrefu, wakati hatuoni matokeo yoyote katika mpira nchini Kenya."}