{"id":1498266,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1498266/?format=json","text_counter":426,"type":"speech","speaker_name":"Jomvu, ODM","speaker_title":"Hon. Twalib Bady","speaker":null,"content":"Hata katika ile Michezo ya Bunge ya Afrika Mashariki inayokuja, Wabunge wote wakifika Mombasa, waangalie kile watakachokitumia na walipe ushuru. Hata kule kukaribishwa na Mama Zamzam mjue sio bure. Mhe. Zamzam, Mama wa Mombasa Kaunti amewakaribisha nyote. Na vile ninavyomjua, mtakula matobosha, viazi vya nazi, samaki wa kupaka na mitai. Mambo mengine ambayo yamesemwa hamna."}