{"id":1507089,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1507089/?format=json","text_counter":137,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Chimera","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Asante, Bw. Naibu Spika, kwa fursa hii. Maoni yangu ni mafupi sana, hususan kuhusu ile hoja ambayo imeletwa hapa na Seneta kutoka Kaunti ya Kajiado, Sen. Seki. Ni kinaya kuona kwamba jamii hii Mbirikani inaweza kupoteza hati miliki ya ardhi yao katika mikono ya maafisa wetu wa usalama."}