{"id":1516473,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1516473/?format=json","text_counter":128,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Wafula","speaker_title":"","speaker":{"id":348,"legal_name":"Davis Wafula Nakitare","slug":"davis-nakitare"},"content":"Bw. Naibu Spika, kwa heshima kuu, ningependa ufafanuzi na maelezo ni lini kiongozi mwenzangu alijiapisha na kujipa mamlaka ya kujitangaza peupe ndani ya Seneti kwamba yeye ni kiongozi na kiti chake kiko wazi upande ule mwingine? Wakenya wasiwe na tabia ya kunyakua uongozi kupitia mlango wa nyuma. Hii ni Seneti na korti iko kule nje."}