{"id":1521087,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1521087/?format=json","text_counter":367,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Mandago","speaker_title":"","speaker":{"id":13577,"legal_name":"Kiplagat Jackson Mandago","slug":"kiplagat-jackson-mandago"},"content":"Mhe. Spika wa Muda, ningeomba Seneta mwenzangu, Madzayo asitumie fursa yake kuwa na ufasaha wa lugha ya Kiswahili kuzuia Waziri kutoa taarifa ambayo inaweza kumfaidi yeye kwa lile swali alilouliza. La pili, Waziri si mmoja wa maseneta katika Jumba hili na kwa hivyo kanuni za Bunge hii haifai kushurutishwa kwa Waziri. Anafaa apewe nafasi ya kujibu swali lililoulizwa."}