{"id":1521939,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1521939/?format=json","text_counter":198,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Ninaomba katika uchunguzi wa suala hili la KALRO, Shirika la Posta pia lijumuishwe. Wanafaa waje kujieleza hapa ni kwa nini wanachelewesha mishahara ya wafanyikazi wao kwa muda wa miezi minne ama mitano. Vile vile malipo ya uzeeni, na ada zingine zinazotozwa wafanyikazi hazipelekwi kwa wakati."}