{"id":1558426,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1558426/?format=json","text_counter":247,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Chimera","speaker_title":"","speaker":null,"content":"Serikali ya Kaunti ya Kwale imejaribu kuipatia ufadhili lakini haujatosheleza timu ile. Kila wikendi, ninapata maombi kutoka kwa maofisa wa klabu kile wakiniomba msaada. Mimi ni mchezaji wa timu ya Bunge FC tukiongozwa na Sen. Cheruiyot. Nimewahi kucheza soka tangu nikiwa kijana mdogo."}