{"id":1558992,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1558992/?format=json","text_counter":232,"type":"speech","speaker_name":"Nakuru County, UDA","speaker_title":"Hon. Liza Chelule","speaker":null,"content":" Asante, Bw. Spika wa Muda. Kama unavyojua, tuko ndani ya Bunge ambapo sisi sote tumechaguliwa na wananchi kuwawakilisha. Hakuna kiongozi anayefaa kumpeleka mwingine shule. Ninazungumza Kiswahili cha nyumbani, na hatuwezi kukilinganisha na Kiswahili cha Lamu au Mombasa."}