{"id":1567671,"url":"http://info.mzalendo.com/api/v0.1/hansard/entries/1567671/?format=json","text_counter":153,"type":"speech","speaker_name":"Sen. Faki","speaker_title":"","speaker":{"id":13211,"legal_name":"Mohamed Faki Mwinyihaji","slug":"mohamed-faki-mwinyihaji-2"},"content":"Bw. Naibu Spika, tuliona pia katika maeneo ya Likoni, Shonda kuna hospitali iliyoanzishwa na ikakamilika, lakini mpaka sasa haijatumika. Wananchi pale wanapata shida kwa sababu zahanati zilizopo pale hazitoshi. Hospitali hiyo ingetoa huduma muhimu kwa wananchi wa sehemu zile."}